Wageni Lyrics – Paul Clement

Katika maisha yangu nilipokea wageni,
Nikawakaribisha kwangu, wakafanya vitu vingi
Hawakuwa wa kudumu, walikuwa wapitaji
Ila moyo wa ukarimu, ukanisababishia machozi

Mgeni wa kwanza alikuwa ni uchungu,
Akaniumiza, akanipa maumivu
Alipomaliza akaenda zake,


Mgeni wa pili alikuwa ni huzuni,
Huyu naye
Akanikosesha furaha,

Mgeni wa tatu alikuwa ni magonjwa,
Akanidhoofisha, akataka kuniua
Hakufanikiwa akaenda zake

Aliyefuata alininyima watoto
Jina lake tasa, naye alipita

Mgeni mmoja jina lake ni mauti
Akamchukua Ntimi, akaniachia jeraha

Mgeni mwingine jina lake hofu
Hakutaka nifanikiwe, akanipa fikra potofu

Nikajiona siwezi, tena nitafeli
Huyo naye alipita

Hawa ni wageni, tena wapitaji
Hawatadumu, watapita
Hawa ni wageni, tena wapitaji
Hawatadumu, watapita

Hakuna jambo lolote gumu
Litakalodumu kwenye maisha yako
Ila yote yatapita
Na yakishapita,
Hayatarudi tena

Tough times never last,
But tough people do

Mapito siyo mambo magumu unayoyapitia kwenye maisha yako,
Ila mapito ni mambo magumu yanayopita kwenye maisha yako,
Ndiyo maana ninaita mapito, kwa kuwa yanapita tu, na yanapita kwenye maisha yako,
Na yakishapita hayawezi kurudi tena, Hah

Magonjwa,
Hao ni wageni, tena wapitaji, Hawatadumu, watapita
Uchungu, (Huzuni)
Hao ni wageni, tena wapitaji, Hawatadumu, watapita
Mateso, (Changamoto)
Hao ni wageni, tena wapitaji, Hawatadumu, watapita
(Hata dhiki)
Hao ni wageni, tena wapitaji, Hawatadumu, watapita

Song by Paul Clement