Nguvu Za Mungu Lyrics – Beda Andrew

Rafiki hivi unavyoniona
Ni kwa neema tu
Na hata uzima nilio nao
Ni upendeleo tu

Na kufika hapa sio sababu ya kuwa
Mimi ni mwema sana (Kuliko wale)
Tena natambua kama si wake mkono
Ningeshatumbukia shimoni na nipotee


Ninalindwa, kwa nguvu za Mungu
Ni kwa nguvu za Mungu
Si kwa ujanja wala akili zangu
Ila ni kwa nguvu za Mungu

Ninalindwa, kwa nguvu za Mungu
Ni kwa nguvu za Mungu
Si kwa ujanja wala akili zangu
Ila ni kwa nguvu za Mungu

Nia ya mwovu ni kutaka ona mi naangamia
Kusudi la Mungu maishani mwangu nisipate timia
Anatega mitego, ili mradi kuniangamiza
Kunimaliza kunipoteza, ila Yahweh ananilinda

Nimeokolewa na ajali
Magonjwa na kila hatari
Mpaka sasa nipo hai
Nakushukuru jemedari

Uzima wangu, hauko mikoni mwangu
Uzima wangu, uko mikononi mwake

Kwa nguvu za Mungu
Ni kwa nguvu za Mungu
Kwa nguvu za Mungu
Ni kwa nguvu za Mungu

Ni kwa nguvu za Mungu
Si kwa ujanja wala akili zangu
Ila ni kwa nguvu za Mungu

Ninalindwa, kwa nguvu za Mungu
Ni kwa nguvu za Mungu
Si kwa ujanja wala akili zangu
Ila ni kwa nguvu za Mungu

Ninalindwa, kwa nguvu za Mungu
Ni kwa nguvu za Mungu
Si kwa ujanja wala akili zangu

Ni kwa neema tu za aliye juu
Aliye juu ni Mungu mkuu
Ni kwa neema tu za aliye juu
Aliye juu ni Mungu mkuu

Ni kwa neema tu za aliye juu
Aliye juu ni Mungu mkuu
Ni kwa neema tu za aliye juu
Aliye juu ni Mungu mkuu

Kwa nguvu za Mungu
Ni kwa nguvu za Mungu
Si kwa ujanja wala akili zangu
Ila ni kwa nguvu za Mungu

Song by Beda Andrew