Amenijibu Lyrics – Gripa Music Feat. Beda Andrew

Jamani nina ushuhuda
Mwenzenu nataka shuhudia
Huyu Mungu ninaye muamini
Alichonitenda nashindwa elezea

Kwa muda mrefu nimekuwa nikiomba
Nikiamini atatenda kwa wakati wake ee
Sababu hawahi wala hachelewi
Akiahidi lazima atende


Yeye ni Mungu wa nyakati
Mungu wa majira
Tena majira sahihi
Jamani namuamini

Kwa muda mrefu nimekuwa nikiomba
Nikiamini atatenda
Na kweli amenijibu
Niliomuomba, niliomuomba

Baba amenijibu
Niliomuomba, niliomuomba yote
Niliomuomba, niliomuomba yote
Niliomuomba, niliomuomba yote

Baba wewe, Yesu wewe
Niliyeitwa mgumba, leo nina mtoto
Kristo kanihurumia na kuniondoa
Kwenye ule msoto

Pia magonjwa na laana
Huyu Yesu kaniondolea
Sasa niko huru, uhuru kweli
Na nimeamini kwamba
Huyu Mungu hawahi wala hachelewi
Akiahidi lazima atende

Yeye ni Mungu wa nyakati
Mungu wa majira
Tena majira sahihi
Jamani namuamini

Kwa muda mrefu nimekuwa nikiomba
Nikiamini atatenda
Na kweli amenijibu
Niliyomuomba, niliyomuomba

Baba amenijibu
Niliomuomba, niliomuomba yote
Niliomuomba, niliomuomba yote
Niliomuomba, niliomuomba yote

Nina furaha moyoni mwangu
Kwa aliyonitenda, huyu Yesu
Nina amani, bwana aliyonifanyia
Mi mwenzenu

Song by Gripa Music Feat. Beda Andrew